Tuesday, March 5, 2013

Sinodi katika Historia ya Kanisa (Pd. Laurenti Magesa)

Pd. Laurenti C. Magesa alikuwa ni mmojawapo wa wawezeshaji katika semina elekezi ya Sinodi ya Jimbo. Katika semina hiyo, alitoa mada kuhusu Sinodi katika Historia ya Kanisa.

Ifuatayo ni mada aliyoitoa kama ilivyokaririwa na Sekretarieti ya Kamati Kuu ya Maandalizi ya Sinodi.

SEMINA ELEKEZI YA SINODI YA JIMBO

Tarehe 21 na 22 Januari 2013 ilifanyika semina elekezi ya Sinodi ya Jimbo katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Mwembeni. Wawezeshaji katika semina hiyo walikuwa ni Pd. Romuald Kajara wa Jimbo la Rulenge - Ngara na Pd. Laurenti Magesa wa Jimbo la Musoma.

Ifuatayo ni hotuba iliyotolewa na Mhashamu Baba Askofu Michael Msonganzila wakati wa ufunguzi wa semina hiyo. Hotuba ya Baba Askofu ilieleza maana na malengo ya sinodi kwa ujumla pamoja na sababu za kuadhimisha sinodi katika jimbo la Musoma.